Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano
Wajumbe wa Kamati za Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano si wafanyakazi wa Baraza. Wajumbe ni wawakilishi kutoka katika asasi za kiraia zilizo mkoani au wilayani.
Baraza limeunda kamati za watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano katika mikoa ya Arusha, Dodoma, Iringa, Lindi, Morogoro, Mtwara, Mwanza, Tanga, Mbeya na Zanzibar
Lengo la Kuundwa kwa Kamati
Lengo kuu la uundwaji wa kamati za watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano ni kuhamasisha watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano nchini kuhusu haki na wajibu wao; pamoja na kukusanya maoni na kero za watumiaji na kuziwasilisha kwa Baraza.
Kazi za Kamati.
Kazi za wajumbe wa Kamati za Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano ni